• Latest News

    Saturday, 24 September 2016

    PREMATURE GRAY HAIR | MVI KABLA YA UZEE




    NOTE!!
    The premature graying problem is largely genetic.
    Hair follicles contain pigment cells that produce melanin, which gives your tresses their color. When your body stops generating melanin, hair presents itself as gray, white, or silver. (Melanin also provides moisture, so when less is produced, hair becomes brittle and loses its bounce.) "If your parents or grandparents grayed at an early age, you probably will too

    Constitutes Hair?
    Before we understand why hair grays, it is important to know about the structure of hair to fully grasp the mechanism behind the graying of hair.
    Hair is a biomaterial composed of a protein called keratin. Hair grows in follicles in the dermis layer of skin. Hair color in humans is found in the hair follicles because of the presence of two types of melanin namely eumelanin and pheomelanin. Generally, the more the melanin, the darker the hair color.
    Normally, it is seen that hair begins to gray on the head, then on the face and slowly progresses to other places like the chest and armpits. This process of graying begins at an average age of 35 years or more and the graying progresses gradually over the years. In some people, the age at which graying starts can differ. For some, graying might begin at an early age and for some it might begin after 40. The difference in the age of graying is dependent on genetics and other factors.
    The majority of people consider gray hair as an indication of old age setting in. However, if you have gray hair at an early age, remember it is not the body that defines the age, it is the mindset.
    Causes for Graying of the Hair
    The dilution of eumelanin and pheomelanin pigments will result ingraying of the hair. To be precise, the melanocytes inside the hair follicles stop producing melanin and this results in graying
    Decrease in melanin is due to the decrease of an enzyme in the body called catalase.
    Catalase breaks down hydrogen peroxide buildup in the body. Due to a decrease in catalase, hydrogen peroxide can suppress the growth of melanin, resulting in graying of the hair.
    Significant amounts of gray hair can appear in younger people too. This phenomenon is called premature graying. Some of the known causes of graying of hair include:
    Sometimes premature graying can run in some families. In other words, genetics does have a role to play in premature graying of hair. Premature graying can be seen in children as young as 12. In some cases, the hair might gray for some time and then turn back into black or natural color as years pass. However, in most cases, graying of the hair continues.
    Emotional Stress
    Emotional stress can lead to premature graying of the hair. Research studies have shown that the release of adrenaline for sustained periods of time had a damaging effect on the DNA, causing it to develop abnormalities. This is also believed to play a major role in graying of hair.
    Diseases:
    Premature graying is seen in the presence of certain diseases related to the thyroid gland such as Grave’s disease, Hashimoto’s disease, hyperthyroidism,hypothyroidism, anemic conditions, and can also appear in skin areas affected by leucoderma. Some people with the condition of vitiligo, where irregular white patches form on the skin have been known to develop early gray hair.
    Improper Diet:
    An improper diet can also be attributed to premature graying of the hair.
    A lack of vitamin B 12, iron, andiodine is considered to be the causes for early graying of the hair. Lack of healthy protein intake is also attributed to early graying of the hair. Tea, coffee, andsmoking may also contribute to early graying.
    Hair Dyes and Hot Water:
    Use of chemical hair dyes and extremely hot water for hair are also considered to cause early graying of hair.
    Age:
    Every decade after the age of 30, the chances of graying hair stand at 10 to 20%.
    There are several home remedies for gray hair that can be easily undertaken without burning a hole in your pocket.These home remedies include:
    Protein intake:
    As hair is made up of protein called keratin, a protein-rich dietwill help increase its production and will improve hair growth. Protein is found in meat, eggs, and cereals, such as wholewheat and lentils.
    Vitamin
    and Mineral Intake: Vitamin A, vitamin B12, iron, copper, and zinc aresome of the very important nutrients.
    Lack of these nutrients may also help in graying of the hair. Food such as meat, poultry, fish (including shell fish), nuts, legumes, raisinand prunes are good sources of these vitamins and minerals.
    Iodine:
    Iodine is a must to stop graying of the hair. Iodine is the element that influences the thyroid gland. Any diseases of the thyroid gland such as hypothyroidism or hyperthyroidism can result in graying of the hair. Iodine is not only found in salt, but also in other foods such as bananas, carrots, and fish.
    Indian gooseberry:
    Indian gooseberry,also known as amla in Hindi, is considered a wonder fruit.
    It is used to treat a variety of ailments in Ayurveda. The dried powder of Indian gooseberry mixed with coconut oil applied on the scalp can be good for graying.
    Consumption of Indian gooseberry improves hair growth and is also good for digestion, respiratorydisorders, diabetes, heart diseases,diarrhea, and dysentery.
    Excessive intake of raw Indian gooseberry is to be avoided. The best way to have it is in powdered form.
    Amaranth:
    The leaves of amaranth or amaranthus are known to be one of the best home remedies for gray hair. The extract from the leaves is helpful in restoring hair color. Apply juice of amaranth leaves to the hair after shampooing and then rinse.
    Black Tea with Salt:
    Applying black tea along with salt is a recommended remedy for gray hair. Take a cup of strong black tea and add a teaspoon of salt. Cool down this solution and apply it on hair roots. Leave it for an hour and then rinse off and do not shampoo it.
    Coconut Oil:
    Many people think this isgrandma’s old trick, but studies have shown that the regular application of oils such as coconut oil help in hair damage and slowing down graying of the hair.
    Avoid Stress:
    Stress is also related to graying of hair. Avoiding or overcoming stress is very important in slowing down the process of graying. Regular exercise,meditation, spending quality time with family and friends can also help.
    Henna:
    Application of henna paste on the hair is another popular home remedy for gray hair. Natural henna paste can be made directly by making a paste of henna leaves with yoghurt and fenugreek seed paste. This paste can then be applied to the hair. It is also used for natural skin dying with no side effects that are usually associated with artificial hair colors.
    Ayurveda:
    In Ayurveda, the ancient science of Indian medicine is stated that a dried powdered mix of Bhringaraja (Eclipta alba), black sesame seeds, and Indian gooseberry in 2:1:1 proportion is good for the hair. This powder must be taken along with milk twice daily for positive results.
    Ginger with Honey Consumption of ginger and honey is also believed to be effective in treating gray hair.
    This mixture has often been prescribed in traditional Chinese medicine.
    Ribbed Gourd:
    Ribbed gourd is another remedy for gray hair. The vegetable should first be cut into pieces, should be shade-dried and boiled with coconut oil and the remaining black residue can be applied on hair roots.
    Cow’s Milk:
    Butter made from cow’s milk is believed to be an effective cure for gray hair. Apply it on the hair roots. The enzymes in cow’s milk and butter are believed to prevent and reverse the process of graying.
    Neem Oil:
    Neem or Azadirachta indica tree is of great significance in
    Ayurveda.
    Essential oil obtained from neem can be used as a remedy for various problems including gray hair. The oil is also helpful for head lice and dandruff. .
    Sesame:
    Sesame seeds, particularly black sesame seeds and sesame oil are also considered good for gray hair, according to Ayurveda. Massage sesame oil on your scalp regularly. One can also include sesame seeds in the diet.
    Chyawanprash:
    Chyawanprash is an Ayurvedic preparation said to be prepared by a sage named Chyawan.
    It is has fruit jam-like consistency. Up to 50 herbal, fruit, oil and spices are added to this mixture. The final product gives various benefits including hair growth. A study conducted by Parle M and Bansal N has emphasized on the benefits of chyawanprash.
    Things to Avoid:
    Smoking, tea and coffee consumption, using strong detergents, very hot water and hot dryers on hair, hair dyes at an early age are some of the things that can be avoided to prevent early hair graying.
    With such remedies in hand, one can make sure that gray hair is a thing of the past.

    Utafiti: Kulala mchana kwa zaidi ya saa moja ni chanzo cha kisukari

    By Ephrahim Bahemu, Mwananchi ebahemu@mwananchi.co.tz
    Kusinzia mchana kwa zaidi ya saa moja ni dalili ya kisukari aina ya pili (type 2 diabetes), utafiti unasema. Utafiti huo wa kwanza wa aina yake umefanywa na wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Tokyo, Japan unabainisha uwekezano huo.

    Watalaamu hao walioongozwa na Dk Yamada Tomahide walipitia tafiti 21 zinazohusianisha kiasi cha usingizi na uwezekano wa kupata magonjwa yasiyo ya kuambukiza; kisukari, shinikizo la damu, magonjwa ya moyo na kupooza ambazo zilihusisha watu 307,237 kutoka bara Asia na nchi za magharibi.
    Watafiti hao waligundua kwamba kusinzia kwa muda unozidi dakika 60 kunaongeza hatari ya kupata kisukari aina ya pili kwa asilimia 45 tofauti na kusinzia kusikozidi dakika 40.
    Uchambuzi wa taarifa walizokuwa nazo wataalamu hao, ulidhihirisha kwamba hakuna hatari yoyote kwa mtu anayesinzia mpaka dakika 40 lakini hatari huongezeka ghafla baada ya kuzidi dakika 60.
    “Utafiti wetu umebaini uwepo wa uhusiano wa kusinzia kwa muda mrefu mchana na uwezekano wa kupata kisukari na magonjwa ya kimetaboliki (metabolic syndrome). Utafiti zaidi unahitajika kujiridhisha kuhusu kusinzia kwa muda mfupi,” ilihitimisha ripoti hiyo iliyowasilishwa kwenye mkutano wa 52 wa Shirika la Utafiti wa Kisukari Ulaya (EASD) uliofanyika Munich, Ujerumani mapema mwaka huu.
    Zipo sababu nyingi zinazoweza kuchangia hatari hiyo. Wanasema usingizi mrefu wa mchana unaweza kumaanisha kuwa mtu hakulala vizuri usiku suala linalohusishwa na msongo wa mawazo ambao ni chanzo cha kisukari.
    Akitoa maoni juu ya majibu ya utafiti huo, Profesa Naveed Sattar, daktari bingwa wa magonjwa ya metaboliki kutoka Chuo Kikuu cha Glasgow, Uingereza anasema: “Utafiti huu unaonyesha uhusiano wa kisukari na usingizi mrefu wa mchana. Inawezekana kinachosababisha kisukari ndicho kinaleta usingizi huo. Inawezekana ni sukari imezidi mwilini hivyo usingizi mrefu kuwa dalili ya kisukari.”
    Profesa huyo, akizungumza na mtandao wa WebMD aliendelea kufafanua kwamba: “Baada ya utafiti huu sasa tunao ushahidi kuwa ukosefu wa usingizi wa kutosha usiku kunahusiana na kisukari. Kinachotakiwa ni kufahamu muda gani unahatari hizo kwa afya ya mtu. Tafiti mpya zitatupa majibu ya kina.”
    Watu wengi wana kawaida ya kujipumzisha mchana. Baadhi ya sehemu, kutokana na majukumu, ni ratiba ya siku kwa watendaji wa aina fulani. Usingizi kiasi pamoja na mlo kamili na mazoezi madogo madogo inafahamika kuwa ni misingi ya afya bora ila utafiti huu unatahadharisha kuwa macho na ule uliopitiliza.
    Pamoja na ukweli huo, usingizi wa mchana unapaswa kuwa mfupi, usiozidi dakika 40. Ushauri huu unatolewa ukiwajumuisha pia wafanyakazi wanaoingia kazini usiku kama wauguzi, madaktari, askari na madereva wa magari ya masafa marefu.
    Dezzy Azimio anasema: “Mara nyingi kama sijaenda kazini huwa nalala au inapotokea sina shughuli ya kufanya. Mara chache huwa nahisi usingizi hata nikiwa kazini hasa baada ya kula.”
    Wataalamu
    Daktari wa Hospitali ya Taifa Mhimbili (MNH), John Seka anakubaliana na majibu ya utafiti huo na anasema kuna uhalisia kwani watu wenye kisukari mara nyingi hujisikia uchovu muda mwingi hivyo kulala muda mrefu, mchana na usiku.
    “Inawezekana utafiti huo ukawa na ukweli kwani baadhi ya watu wenye matatizo ya kuchoka mwili ambayo husababisha walale mara kwa mara huwa na hali za kukojoa na kiu ambazo ni dalili za kisukari,” anasema Dk Seka na kuongeza:
    “Wagonjwa wanaokuja hospitali kwa malalamiko ya uchovu wa mwili, wakiulizwa dalili nyingine walizonazo huwa wanazitaja za kisukari na hata ukimpima unakuta tayari ana kisukari aina ya pili.”
    Mtaalamu wa tiba ya kisukari kutoka Hospitali ya Mwananyamala, Dk Nurdin Mavura anasema kuna uhusiano mkubwa na hata madaktari wa nchi nyingine walishafanya utafti huo na kubaini hilo.
    “Mtu anaposinzia kongosho lake huwa halifanyi kazi ya kupunguza au kuongeza sukari wala sukari iliyopo haitumiki mwilini kwa muda. Hivyo basi kama usingizi utakuwa wa muda mrefu ni rahisi kwake kupata kisukari,” anasema Dk Mavura.
    “Watu wanaougua magonjwa yanayowalazimu kulala muda wote nao wapo kwenye hatari ya kupata kisukari kwa kuwa mwili haujishughulishi kuondoa mafuta ya ziada ambayo hutokana na kukaa bila kufanya mazoezi ukija kuwapima unakuta tayari wanaumwa kisukari.”
    Dk Mavura aliongeza kuwa siyo watu wanaosinzia kwa muda mrefu mchana peke yao waliopo kwenye hatari hiyo ya kupata kisukari aina ya pili bali hata wale ambao hukaa muda mwingi au kutembelea sana gari na kukosa muda wa kufanya mazoezi kwa muda mrefu.
    Kifahamu kisukari aina ya pili
    Awali ugonjwa wa kisukari aina ya pili ulijulikana kama aina ya kisukari kisichotegemea insulini au kisukari kinachoanza katika utu uzima.
    Lakini ugonjwa huo ni tatizo la kimetaboliki linalotambulika kutokana na kiwango cha juu cha glukozi katika damu katika muktadha wa kukinza insulini na upungufu wa insulini kwa kiasi kidogo.
    Ugonjwa huu huu ni kinyume na kisukari aina ya kwanza ambacho kinatokana na upungufu wa insulini kufuatia kuharibika kwa seli za endokrini katika kongosho.
    Dalili zake huwa ni kuu ni kiu mara kwa mara, kukojoa kila mara na kuhisi njaa kila wakati.
    Kisukari aina ya pili huchangia hadi asilimia 90 ya visa vya kisukari huku asilimia 10 iliyosalia ikisababishwa na kisukari aina ya kwanza na kisukari katika ujauzito.
    Unene wa kupindukia unaelezwa kuwa ni miongoni mwa sababu zinazochangia kisukari aina ya pili.
    Hata hivyo, wataalamu wanashauri kula chakula kwa kiasi na kufanya mazoezi ya mara kwa mara ili kupunguza hatari iliyopo. Endapo dalili zitajitokeza, mgonjwa anashauriwa kwenda hospitali mara moja ili kupata maelekezo ya kitaalamu kabla hali yake haijawa mbaya.
    Kisukari kinatakiwa kutibiwa mapema ili kuepuka madhara yake. Watalaamu wanaelezwa kwamba kisukari aina ya pili kinaweza kusababisha magonjwa ya moyo, kiharusi, kupungua kwa uwezo wa kuona, matatizo ya figo na kuathiri mzunguko wa damu.

    DEPRESSION | Sonona tatizo la kiafya lisilopewa uzito na wanajamiii


    By Dr.Shita samwel, Mwananchi
    Yapo matatizo ya kiafya ambayo jamii imekuwa ikiyapuuza kuwa siyo changamoto kubwa. Mojawapo ni Sonona ingawa kwa lugha ya kitabibu hujulikana kama Depression.

    Tatizo hili huathiri afya ya akili na mwili kwa ujumla. Takwimu zinaonyesha kuwa athari zake hujitokeza kwa asilimia 10 ya jamii fulani duniani. Mara nyingi, huwakumba zaidi watu wenye umri kati ya miaka 10 na 24.
    Depression kama wengi walivyozoea ni tatizo linalosababisha kushuka kwa hisia au mihemko ya kimwili hivyo mhusika kutojihusisha na shuguli yoyote suala linalomuathiri kimawazo, kitabia na hisia za mwili na kutojiona sawa kama walivyo watu wengine wanaomzunguka.
    Mtu mwenye Sonona hukosa furaha, huwa muoga na kukosa matumaini. Mara kadhaa huwa hana msaada, hukerwa bila sababu za msingi, hujiona mkosefu, mwenye kuaibisha na asiye mtulivu.
    Mtu mwenye tatizo hili anaweza pia kukosa hamu ya kujishughulisha na chochote ikiwa ni pamoja na kufanyakazi ambayo awali alikuwa akiipenda na kuifurahia.
    Vilevile anaweza kukosa hamu ya kula au kula kupita kiasi. Anakosa umakini wa mambo, anashindwa kukumbuka masuala binafsi kwa kina na pia na mara nyingine akawa na tabia za kujaribu kujiua.
    Mambo mengine yanayoweza kumpata mtu huyu ni kukosa usingizi, kulala kulikopitiliza, mwili kuumwa na uchovu mkali. Wakati mwingine huweza kuwa na matatizo ya usagaji chakula au nguvu za mwili kupungua.
    Kupata Sonona ni zaidi ya kuwa na huzuni, kwa maana nyingine ni kukosa raha kulikopitiliza. Tatizo hili linamtokea mtu akiwa amepata dalili hizi mfululizo kwa zaidi ya wiki mbili.
    Sababu zinazochangia kutokea kwa tatizo hili ni zile za kimwili (kibailogia) na kisaikologia. Kimwili ni pamoja na mabadiliko katika ubongo, kemikali zinazosafirisha taarifa na homoni (lakini bado haijulikani kwa kina sababu zakibailogia/kimwili zinavyosababisha sonona kutokea).
    Mazingira tunayoishi ndiyo huwa chanzo cha matatizo ya kisaikolojia ambayo huweza kuwa kufiwa au kumpoteza mtu wa karibu, kupoteza kazi, kufilisika, kupokea taarifa mbaya na kuwa katika mazingira magumu.
    Endapo hatua za makusudi hazitachuliwa kwa haraka mhusika huwa kwenye hatari ya kujiua au kuchanganyikiwa kiasi cha kupata uwendawazimu wa kudumu.
    SourceMwanchi

    Hata watu wazima huugua homa ya mapafu (PNEUMONIA)

    By Jackline Masinde, Mwananchi jmasinde@mwananchi.co.tz
    Mapema mwezi huu, mgombea urais wa Marekani kwa tiketi ya chama cha Democratic, Hillary Clinton alilazimika kurekebisha ratiba yake baada ya afya yake kutetereka ghafla, hivyo kuhitaji huduma za kitabibu. Ni baada ya kushambuliwa na ugonjwa wa homa ya mapafu (pneumonia) unaoenezwa kwa njia ya hewa.

    Taarifa za timu yake ya kampeni zilisema mgombea huyo alikuwa amechemka, hivyo kuongezewa maji na kupewa dawa na kushauriwa apumzike.
    Daktari wake, Lisa Bardack alithibitisha hayo na kusisitiza kuwa Hillary anaendelea vizuri.
    “Nilishauriwa nipumzike kwa siku tano lakini sikuzingatia ushauri huo. Nataka nimalizane na hili suala ili nirudi kwenye kampeni mapema iwezekanavyo,” alisema Hillary akikaririwa na gazeti moja.
    Pneumonia hutokana na kuvimba kwa mkusanyiko wa seli katikam moja au mapafu yote mawili. Mara nyingi husababishwa na bakteria. Mwishoni mwa mirija ya kupumulia mwa mapafu yote, kuna mifuko midogo. Unapokuwa na homa ya mapafu, mifuko hiyo huvimba na kujaa maji na hivyo kusababisha ugumu katika kupumua, homa, kukohoa, kutoka jasho kutetemeka au kupoteza jamu ya kula.
    Watu wa umri wowote huugua pneumonia, lakini ugonjwa huo huwakumba sana watoto na wazee wenye umri zaidi ya miaka 65
    “Mwanangu aliwahi kuugua na tulilazwa hospitali. Sifahamu kama watu wazima nao wanaugua. Sijawahi kuona,” anasema Jackline Champanda .
    Homa ya mapafu husababisha vifo vingi duniani.
    Takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonyesha kuwa asilimia tano ya vifo vya watoto vilivyotokea mwaka 2008 vilisababishwa na pneumonia. Mwaka huo ugonjwa huo ulisababisha vifo vya zaidi ya watu 675,000 duniani.
    Katika kukabiliana na ugonjwa huo, Shirikisho la Kimataifa la Wafadhili wa Chanjo Duniani (Gavi) linatoa chanjo ya pneumonia (pneumococcal vaccines) kwa nchi zaidi ya 50 zinazoendelea. Tangu mwaka 2010, shirikisho hilo limetoa chanjo kwa zaidi ya watoto milioni 47 huku idadi ya watoto walionufaika kwa chanjo nyinginezo wakifika milioni 277 kuanzia mwaka 2011 mpaka 2015.
    Gavi na WHO zinatoa chanjo hizo kwa wote wanaohitaji. Watoto hupata chanjo mara tatu; wakiwa na wiki nane tangu kuzaliwa, wiki 16 na ya mwisho wanapotimiza umri wa mwaka mmoja. Wazee na wenye magonjwa sugu hupewa mara moja na kuzuia kwa kiasi kikubwa uwezekano wa kupata tena maambukizi hayo.
    Wengine ambao wako hatarini kupatwa na ugonjwa huo ni watumiaji wa dawa za kulevya.
    Takwimu zinaonyesha watu wanane kati 1,000 nchini Marekani husumbuliwa na maambukizi haya ambayo hutokea zaidi wakati wa kipindi cha baridi kali.
    Wataalamu
    Mtaalamu wa magonjwa na saikolojia ya tiba kutoka Hospitali ya Kinondoni, Adili Kadria anasema nimonia inatokana na hiitilafu zinazotokea katika sehemu moja au mbili za mapafu.
    “Inaweza kuwa ni uvimbe ambao husababishwa na bakteria au virusi vinavyoenezwa kwa njia ya hewa na kuifanya mishipa ya kupitisha hewa kushindwa kufanya kazi kutokana na kujaa maji,” anasema Kadria.
    Daktari wa Hospitali ya Mkoa wa Geita, Adamu Sijaona anasema nimonia ni ugonjwa unaosababishwa na aina fulani ya seli nyeupe za damu ziitwazo eosinofil ambazo hukusanyika kwenye mapafu.
    Dalili
    Dk Kadria anasema dalili za awali za nimonia huanza kuonekana ndani ya saa 24 mpaka 48. “Moja ya dalili hizo ni kukohoa. Mgonjwa anaweza kutoa makohozi mazito ya rangi ya njano au kikohozi kikavu,” anasema.
    Wataalamu wa afya wanaziweka dalili za nimonia kwenye makundi mawili; za jumla na zile za hatari ambazo mgonjwa anahitaji msaada wa daktari haraka.
    Kwa mujibu wa Hospitali ya Chuo Kikuu cha Merland, Marekani, dalili za jumla hutofautiana kulingana na umri. Kwa ujumla wake, dalili hizi huonekana kwa watoto, watu wazima au wazee na zinajumuisha homa inayoambatana na kutetemeka mwili na maumivu ya kifua hasa upande wa pafu lililoumia.
    Nyingine ni kikohozi kikavu, kutokwa jasho hasa usiku, kichefuchefu, kutapika na maumivu ya misuli. Mgonjwa pia anaweza kuhisi mapigo ya moyo na pumzi kwenda kasi, kukata pumzi kukichukua muda mrefu kidogo basi uzito unapungua.
    Dalili za hatari zinazohitaji huduma za haraka za daktari ni pamoja na homa kali, kushindwa kupumua na rangi ya ngozi kuwa ya bluu. Nyingine ni kikohozi cha makohozi kutoka ndani, kupoteza kumbukumbu hasa kwa wazee, kupungua uzito ndani ya muda mfupi na mapigo ya moyo kwenda kasi.
    Aidha, Dk Kadria anasema mgonjwa anaweza kubanwa na kifua, kuhisi maumivu ya kichwa na kupoteza hamu ya kula.
    Dk Sijaona anasema: “Watu wanaoshambuliwa zaidi ni wale ambao kinga zao za mwili ni dhaifu. ”
    Wataalamu wanasema mgonjwa anahitaji matibabu kwani akiachwa kwa muda mrefu anaweza kusababishiwa kifo. Wanasema vijana wanaweza kupona bila kupatiwa matibabu endapo watakunywa maji mengi.
    Kinga
    Nimonia unasababishwa na bakteria au virusi na namna ya kwanza ya kuuepuka ni kuzingatia usafi. Mgonjwa anashauriwa kutumia kitambaa kisafi kila anapokohoa au kupiga chafya na kujifuta. Anashauriwa kukitupa kitambaa kilichotumika kwani wadudu wanaweza kukaa humo kwa muda. Vilevile mgonjwa anashauriwa kunawa mikono ili asiwaambukize wengine vimelea vya ugonjwa.
    Kulinda afya kwa kuepuka matumizi ya sigara kunakoathiri mapafu na kutoa mwanya wa maambukizi kunasaidia kutoshambuliwa na ugonjwa huo.
    Njia ya uhakika ya kukabiliana na nimonia ni chanjo ambayo hutolewa kwa watoto na wazee. Watoto wenye umri chini ya miaka mitano hupewa Pneumococcal Conjugate Vaccine (PCV13) wakati wazee wenye zaidi ya miaka 65 hupewa Pneumococcal Polysaccharide Vaccine (PPSV23).
    Tahadhari
    Wataalamu wa afya wanansema ugonjwa huu unaotibika endapo muathirika atawahi hospitali na atazingatia ushauri wa daktari. Kupumzika muda wa kutosha na kunywa maji mengi au juisi ya matunda inasaidia kupunguza madhara ya ugonjwa huu.
    Mgonjwa asiye na maambuki mengine, inaelezwa kuwa anaweza akapona kwa kuzingatia masuala yaliyobainishwa hapo juu na kujiepusha na mazingira hatarishi. Watu wenye upungufu wa kinga wanashauriwa kukaa mbali na mgonjwa wa nimonia mpaka atakapopona kabisa ili kuepuka maambukizi mapya.
    Mikusanyiko ya watu, wataalamu wanabainisha, ni miongoni mwa mazingira rahisi kwa mtu kupata maambukizi hayo. Daktari bingwa wa mapafu wa Hospitali ya Cleveland, Wayne Tsuang alipohojiwa na mtandao wa WebMD juu ya kuanguka kwa Hilary alisema huenda mgombea huyo wa Urais alikuwa walking pneumonia ambayo mgonjwa anakuw ahajitambui kama anayo.
    “Inawezekana alikuwa na aina hiyo. Aina hii ya nimonia inasababishwa na bakteria waitwao mycoplasma. Mara nyingi huwashambulia vijana na inaweza ikawepo kwa wiki kadhaa lakini hupona kabla ya kutibiwa. Wengi hupona bila kutibiwa,” alikaririwa Dk Tsuang na kufafanua kuwa ni asilimia 50 ya wagonjwa wa nimonia ndiyo hugundulika ila wanaobaki hutibiwa dalili zake tu.
    Source Mwananchi

    Kuwa makini na maambukizi ya sikio kila unapoenda kuogelea

    By Cledo Michael, Mwananchi Mwananchipapers@mwananchi.co.tz
    Sylvia Mtenga (22), mwanafunzi wa chuo kikuu jijini Dar es Salaam anasema anapenda kuogelea na hufanya hivyo kila anapopata nafasi hasa siku za mwisho wa wiki.

    “Mimi na marafiki zangu tunapenda kushindana kuogelea. Tunajisikia vizuri. Hatufanyi hivyo kwa lengo la kujiandaa na michuano ila ni wa afya zetu,” Sylvia.
    Watanzania wengi wanapenda kuongelea kutokana na uwepo wa mazingira rafiki ya kufanya hivyo. Wingi wa mabwawa na mito ya asili, maziwa na Bahari ya Hindi ni miongoni mwa vitu vinavyowafanya wengi wauupende mchezo huo kama ilivyo kwa Sylvia.
    Fukwe za bahari na maziwa ni miongoni mwa sehemu zinazotembelewa na watu wengi kwa ajili ya burudani hiyo. Hoteli nzuri zimejengwa maeneo hayo kutokana na kivutio hicho kwa lengo la kupata wateja wengi.
    Mabwawa ya kuogelea pia yapo kwenye hoteli nyingi zenye hadhi ya juu ambako watoto wakiwa chini ya uangalizi wa familia au walimu hupenda kutembelea na kuogelea. Licha ya matukio kadhaa ya watoto kuathirika na wakati mwingine kupoteza maisha kutokana na kukosa uangalizi makini, maji yana athari sikioni.
    Kwa wanaopenda kuogelea ni kawaida maji kuingia sikioni ingawa hutoka baada ya muda. Maji hayo yanaelezwa husababisha maambukizi ya sikio na inashauriwa kuwa makini zaidi ili kuepuka madhara.
    Maambukizi ya sikio ni kitu ambacho kila mwogeleaji; mzoefu au anayejifunza anapaswa kuwa makini nayo. Wataalamu wa kuogelea wanasema, mara nyingi, maji huingia sikioni wakati wa anapopiga mbizi au anapozama na kuibuka.
    Maji yakiingia sikioni, mhusika anasika maumivu au anapoteza usikivu kwa muda mpaka yatakapotoka. Ushauri unatolewa ili kuepuka jambo hili kwa usalama wa masikio na afya ya waogeleaji.
    Mtaalamu
    Mtaalamu wa afya kutoka Chuo Kikuu cha Afya Muhimbili (Muhas), Dk Benjamini Rulakuze anaeleza kuhusu maambukizi ya sikio kwamba yanasababishwa na bakteria au fangasi waishio ndani ya maji.
    Anasema mara nyingi maji huwa na bakteria au fangasi na ndiyo maana mabwawa husafishwa mara kwa mara iki kuwaondoa na kuhakikisha afya ya muogeleaji na kumwepusha na maambukizi ya sikio ambayo kitaalamu hujulikana kama Otitis Externa ambayo husababishwa na bakteria waitwao Staphylococcus Aureas au Pseudomanas Auriginosa.
    Anasema maji yakiingia sikioni huondoa utando au nta iliyomo ambayo kazi yake kubwa ni kuua bakteria na kunasa na kuutoa uchafu uingiao hivyo kuruhusu bakteria kuishi na kusababisha maamubukizi. Anafafanua kuwa maambikizi haya hayasababishwi na kuogelea pekee bali kuna vitu vingine vinavyochangia mfano matumizi ya pamba za kusafishia masikio (cotton buds) pia huweza huondoa nta hiyo vilevile.
    Anazitaja dalili za ugonjwa huu kuwa ni pamoja na sikio kuuma hasa likiguswa sehemu ya nje, kutosikia vizuri na kutokwa uchafu au usaha. Anashauri kila anayeona dalili hizi kupata ushauri wa kitaalamu kabla hali yake haijawa mbaya zaidi na uwezekano wa muleta madhara makubwa.
    “Hospitali kuna vifaa maalumu vya kusafishia sikio lenye tatizo kabla dawa zinazohitajika hazijatolewa. Mtu anayechelewa kupata matibabu anaweza kuathirika zaidi na kusababisha maambukizi hayo kupanda hadi kwenye ubongo na kuotesha jipu hatua ambayo ni mbaya na inahitaji upasuaji ili kutibu,” anasema.
    Ushauri
    Ili kuepuka madhara ya muda mrefu yanayoweza kusababishwa na maambukizi hasa kutokana na maji wataalamu na wadau wa afya wanashauri kila mtu kuwa makini anapoogelea, huku msisitizo ukielekezwa zaidi kwa watoto.
    Chama cha Msalaba Mwekundu nchini Marekani kinaeleza masuala muhimu ya kuzingatia kabla na wakati wa kuogelea ili kuepuka madhara yoyote yanayoweza kujitokeza kwa wapenzi wa burudani hiyo.
    Usalama wa maisha
    Miongoni mwa mambo muhimu kuzingatia wakati wa kuogelea, iwe bwawani, ziwani au baharini usalama ni jambo muhimu. Kila mtu anatakiwa kuogelea kwenye eneo lisilo hatari kwake. Lisiwe lenye kina kirefu kitakachomshinda kujiokoa ikihitajika.
    Eneo lenye watoto au waogeleaji wanaojifunza linatakiwa kuwa na usimamizi. Watoto wanapaswa kufundishwa na kuengewa utamaduni wa kuomba watoto kuomba ruhusa kabla ya kwenda kuogelea na kamwe usiwaache peke yao.
    Maboya ya kujiokolea
    Watoto wadogo na wasiokuwa na ujuzi wa kuogelea wanatakiwa wavae maboya ya kuogelea muda wote wanapokuwa kwenye maji. Licha ya maboya hayo watoto na wanaojifunza kuogelea wanatakiwa kuwa chini ya uangalizi.
    Jifunze kuogelea kwa ustadi
    Kuogelea ni taaluma na mchezo wenye kanuni za umahiri. Kabla ya kuwa na ujuzi utakaokufanya ufurahie zaidi, inashauriwa kujiunga na madarasa yanayofundisha uogeleaji.
    Muda wote wa kufanya hivi inashauriwa kujiepusha na unywaji wa pombe au matumizi ya kilevi cha aina yoyote. Pia, hata baada ya kuwa mahiri kwenye uogeleaji haishauriwi kuogelea ukiwa umelewa.
    Usalama wa bwawa
    Kwa wanaomiliki mabwawa nyumbani au sehemu nyingine yoyote wanashauriwa kuhakikisha yanakuwa na mipaka ya kina au vizuizi na vifaa sahihi vya msaada na kujiokolea pindi utakapohitajika.
    Vifaa hivyo vinaweza kuwa maboya ya kuogelea sanduku la huduma ya kwanza na simu kwa ajili ya mawasiliano ya dharura. Namba za dharura kwa msaada wa haraka zinapaswa ziwekwe sehemu ambayo kila mtumiaji wa bwawa husika ataziona kwa urahisi na kuweza kuzitumia na kupata msaada unaohitajika kwa wakati.
    Ulinzi uzingatiwe wakati wote watoto wanapocheza kwenye maji na endapo kuna mmoja kati yao anakosekana au kupungua ni vema akatafutwa haraka kwa kutazama ndani ya maji kwanza kwani sekunde moja inaweza kusababisha kifo au ulemavu kwa watoto.
    Tahadhari
    Wataalamu wanapendekeza matumizi ya taulo au nguo kukausha sikio baada ya kuogelea badala ya pamba za masikio au vijiti. Wanatahadharisha matumizi ya pamba kwa sababu inaweza kuharibu ngoma ya sikio au kuondoa nta hivyo kuchangia tatizo kubwa kuliko ilivyotarajiwa.
    Wataalamu wanashauri kuwa ni vyema kutumia vifaa maalumu vya kuogelea vinavyokinga macho na masikio dhidi ya hatari itokanayo na maji machafu wakati wa kuogelea.
    Elimu juu ya magonjwa bado inahimizwa na wataalamu wengi ili watu waweze kujikinga dhidi ya maradhi yanayoweza kuepukika kuliko kusubiri tiba.
    Source Mwananchi

    Mambo yanayosababisha uvimbe wa kidoletumbo

    By Clifford Majani, Mwananchi
    Kidoletumbo maarufu kama Apendeksi ni sehemu ya utumbo iliyo na umbo kama kidole na uwazi kama bomba ambayo inaning’inia katika makutano ya utumbo mdogo na  mpana, upande wa kulia, chini ya tumbo kati ya kitovu na nyonga.
    Kwa wastani, kidoletumbo kina urefu wa sentimeta tisa ingawa kinaweza kuwa na urefu wowote kati ya sentimeta mbili hadi 20 kwa baadhi ya watu.

     Historia ya utabibu inaonyesha kuwa kidoletumbo kirefu zaidi ni kile kilichoonekana kwa mgonjwa aliyefanyiwa upasuaji huko Zagreb, nchini Croatia ambacho kilifika urefu wa sentimeta 26.  Inakadiriwa kuwa, kipenyo cha kidoletumbo ni kati ya milimeta saba mpaka nane.
    Kiungo hiki kinaweza kuathiriwa na vitu mbalimbali na kusababisha kuvimba, ugonjwa ambao uligunduliwa kwa mara ya kwanza na Dk Robert Lawson Tait mwaka 1886, na tangu hapo madaktari wamekuwa wakiutibu kwa upasuaji wa kukiondoa kiungo hicho.
    Kidoletumbo husaidia katika mmeng’enyo wa chakula na uzalishaji wa kinga za mwili ambazo husaidia kupambana na kuua baadhi ya vimelea vya maradhi vinavyoingia katika tumbo kupitia chakula.
    Utafiti wa kitabibu uliofanyika katika Hospitali ya Chuo Kikuu cha Winthrop iliyoko New York Marekani, na kuchapishwa mwaka 2011 katika jarida la Clinical Gastroentorology and Hepatology toleo namba 9, ulionyesha kuwa watu ambao hawana kidoletumbo walikuwa wanakabiliwa na hatari ya kupata uvimbejoto wa utumbo unaosababishwa na bakteria aina ya Clostridium difficile, mara nne zaidi wakilinganishwa na wenye nacho.
    Utafiti mwingine uliofanywa mwaka 2007 na profesa wa upasuaji, Dk William Parker pamoja na jopo la wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Duke, ulibainisha kuwa kidoletumbo huhifadhi  bakteria rafiki kwa binadamu wanaosaidia umeng’enyaji au ulainishaji wa vyakula vya nyuzilishe (fibres) ambavyo tunakula kila siku.
    Utafiti huo unaonyesha kuwa bakteria hawa hupotea kwa wingi wakati binadamu anapopata maradhi ya kuharisha, kipindupindu na kuhara. Wale wanaobaki salama ndani ya kidoletumbo, huzaliana na kurudi katika utumbo ili kusaidia mwili uendelee na kazi zake.
    Pamoja na faida zake, Profesa Parker anasema haimaanishi kuwa ni lazima kidoletumbo kiendelee kuwapo kwa gharama yoyote. Muhimu watu wakaelewa kwamba hawana sababu ya kuking’angania kidoletumbo kilichovimba.
    “Hatutaki matokeo ya utafiti wetu yasababishe madhara. Watu wasiseme, kidoletumbo changu kina kazi muhimu hivyo siendi kwa daktari. Nitajaribu kukilinda ili kisitolewa,” anasena Profesa Parker.
    Ugonjwa wa kuvimba kwa kidoletumbo unaweza kuathiri mtu wa rika lolote, lakini wale wenye umri kati ya miaka 15 hadi 30 wana na uwezekano mkubwa wa kupatwa na tatizo hili. Pamoja na hali hiyo, inasemekana kuwa wanawake wana uwezekano mdogo wa kuugua ugonjwa huu ikilinganishwa na wanaume. Wataalamu wa afya pia wanabainisha kwamba siyo rahisi kwa watoto chini ya miaka miwili kupatwa na ugonjwa huu.
    Uvimbe wa kidoletumbo ukikaa muda mrefu, huzuia mzunguko wa damu hivyo kusababisha kuta zake kuoza na kutunga usaha. Hali hii husababisha uvimbe wa ngozi laini inayofunika tumbo na kutokeza maumivu makali ya tumbo lote. Iwapo mgonjwa atachelewa kupata tiba sahihi, uambukizo kutoka katika uvimbe wa ngozi laini inayofunika tumbo husambaa katika mfumo wa damu na kusababisha matatizo mengine makubwa zaidi. Tatizo hilo linaweza kuwa baya zaidi endapo kidoletumbo kitapasuka kwani mgonjwa anakuwa katika hatari ya kupoteza maisha.
    Tafiti mbalimbali za kitabibu ikiwa ni pamoja na ule uliochapishwa mwaka 2010 katika jarida la ‘Infectious Disease Clinics of North America’ toleo namba 24(4), zinaeleza kuwa uvimbe husababishwa na maambukizi ya bakteria, fangasi, virusi na minyoo kama vile kichocho, Enterobius vermicularis, Strongyloides stercoralis na minyoo mikubwa. Vilevile, tatizo hili linaweza kusababishwa na uvimbe kwenye tishu za limfu au wowote katika utumbo.
    Kwa kuwa sehemu hii ya utumbo hupitiwa na chakula kilichoyeyushwa, inaweza kuzibwa endapo chakula hicho kitakuwa na mchanga au vitu vidogovidogo ambavyo ni vigumu kama vile nyama zisizotafunika au mbegu za matunda ambazo hujikita ndani na kushindwa kutoka. Wachunguzi wa mambo ya mfumo wa chakula wanadai kuwa asilimia tano ya vitu vigumu ambavyo mtu anaweza kumeza lakini visiyeyuke, vinaweza kujikusanya katika sehemu ya chini ya utumbo mpana na kuingia katika kidoletumbo.
    Matokeo ya utafiti uliofanyika nchini Uturuki na kuchapishwa katika jarida la Asian Pacific Journal of Tropical Biomedicine, toleo namba 1(2) la mwaka 2011, yalionyesha kuwa mbegu za matunda na taka ngumu zinazotokana na mabaki ya chakula, zinaweza kusababisha uvimbe wa kidoletumbo. Taka hizo ngumu zinapojikusanya kwenye kidoletumbo au kuganda na kushindwa kutoka, huanza kuchochota, kuvimba, kupata maambukizi ya bakteria na hatimaye kusababisha maumivu makali kwa muhusika.
    Dalili kuu ya ugonjwa huu ni maumivu makali ya tumbo ambayo huanzia katikati ya tumbo, eneo la kitovu na ambayo hudumu ndani ya saa moja au zaidi na baada ya hapo huhamia upande wa kulia, chini ya tumbo ambako ndiko kidoletumbo kilipo. Maumivu haya yanaweza kuwa makali zaidi wakati wa kupiga chafya, kukohoa au kutembea. Dalili nyingine zinazoweza kujitokeza ni pamoja na kuhisi homa, kufunga choo, kichefuchefu na kuharisha.
    Uchunguzi wa kitabibu wa ugonjwa huu unategemea maelezo na historia ya mgonjwa, dalili zinazojitokeza. Vipimo vya damu na mkojo wa mimba kwa wanawake wenye umri wa kuzaa pia vinaweza kufanyika pamoja na vipimo vya CT scan na Ultrasound ya tumbo ili kuweza kubaini hali na ukubwa wa tatizo la kidoletumbo. Hakuna kipimo rahisi na cha moja kwa moja kinachoweza kuthibitisha haraka ugonjwa wa kidoletumbo kwa wanawake hasa wakiwa wajawazito.
    Kutokana na hali hiyo iwapo daktari ataona dalili za wazi baada ya kubaini sehemu yenye maumivu tumboni, anaweza kuamua kufanya upasuaji wa tumbo haraka ili kuondoa kidoletumbo kilichovimba, kuziba au kuoza. Lakini mgonjwa anaweza kufanyiwa upasuaji baada ya kuelezwa hali halisi ya tatizo lake na kusaini fomu za kukubaliana na tiba ya upasuaji ili kuokoa maisha yake kutokana na hali aliyonayo. Mgonjwa anaweza kupewa matibabu ya dawa za kundi la antibaiotiki kwa kudungwa sindano ambazo zinaweza kuuwa bakteria wanaoshambulia kidoletumbo.
    Kutokana na hatari zinazoambatana na tatizo hili, mgonjwa anashauriwa kuwahi mapema kituo cha afya mara anapoona dalili. Ni busara kuepuka matumizi ya dawa za asili na tiba mbadala kama baadhi ya watu wanavyofanya pindi wanapohisi maumivu makali ya tumbo jambo ambalo linaweza kuhatarisha afya na maisha yao.
    Ingawa ni vigumu kujikinga na kuepuka hali hii, lakini ni vyema kutambua kuwa katika jamii zinazotumia vyakula vyenye nyuzilishe, matunda na mbogamboga kwa wingi, tatizo hili halitokei mara kwa mara. Pia ni busara kujiepusha na utumiaji wa vyakula vyenye mchanga kama vile mchele na dagaa wanaokaushwa na kuhifadhiwa katika hali duni. Vilevile, inashauriwa kuepuka kuweka mdomoni vitu vigumu, ambavyo si chakula vinavyoweza kumezwa. Wataalamu pia wanashauri kwamba wakati wa kula ni vyema chakula kitafunwe vizuri kabla ya kumeza.
    Source Mwananchi

    Maambukizi Sugu ya Njia ya Mkojo (Chronic UTI) ni Nini?

    By Joachim Mabula, Mwananchi
    Yapo maambukizi ambayo hayatibiki kwa urahisi au yanajirudia mara kwa mara licha ya kutibiwa. Maambukizi sugu ya njia ya mkojo (Chronic Urinary Tract Infections (UTIs)  ni miongoni.
    Njia ya mkojo ni sehemu ya mfumo wa mkojo wenye ogani mbalimbali kama figo, urethra (mirija inayobeba mkojo kutoka kwenye figo kwenda kwenye kibofu cha mkojo).
    Maambukizi kwenye njia ya mkojo yanaweza kutokea sehemu yoyote katika mfumo huu. Ikiwa maambukizi yataathiri kibofu cha mkojo peke yake ni rahisi kutibika lakini yakisambaa mpaka kwenye figo, mwathirika huumwa zaidi na pengine kulazwa hospitali.

    Ingawa maambukizi ya njia ya mkojo yanaweza kumpata mtu yeyote kwa wakati wowote, sanasana wanawake. Utafiti wa National Institute of Diabetes and Digestive and Kidney Diseases (NIDDK) inakadiria kuwa katika kila wanawake watano, mmoja ana maambukizi sugu ya njia ya mkojo yanayojirudia mara kwa mara.

    Kinachoongeza hatari ya maambukizi sugu ya njia ya mkojo
    Maumbile: Maambukizi sugu ya njia ya mkojo huwapata sana wanawake kutokana na maumbile yao.
    Kwanza, urethra yao ipo karibu sana na puru (rectum) hivyo kurahisisha bakteria kutoka kwenye puru kuingia kwenye urethra hasa wakati wa kutawaza. Mara nyingi hutokea endapo mhusika atajisafisha kwa kurudisha mkono kutoka nyuma kwenda mbele. Watoto wadogo wa kike hupata maambukizi ya UTI kwa kuwa hawaijui kanuni hii.
    Pili, urethra ya mwanamke ni fupi zaidi ikilinganishwa na ya mwanaume. Bakteria wana umbali mfupi wa kusafiri kufika kwenye kibofu cha mkojo ambako wanaweza kuzaliana na kuongezeka kiurahisi na kusababisha maambukizi.
    Aina ya Maisha: Kuna aina ya maisha ambayo yanaweza kukufanya uwe kwenye hatari zaidi ya kupata maambukizi kwa urahisi. Kwa mfano kutumia diaphragm (mpira laini maalumu unaowekwa ukeni wenye kizibo cha kuzuia mbegu za mwanamme kupenya ili  kukutana na yai la mwanamke) inaweza kusukuma juu urethra na kufanya iwe vigumu kutoa mkojo wote baada ya kukojoa. Mkojo unaobaki kwenye kibofu huongeza uwezekano wa bakteria kuzaliana na kusababisha maambukizi.
    Vilevile, matumizi ya vitu vyenye kemikali kuosha uke vinavyoua bakteria walinzi wa kwenye uke, kama sabuni, marashi au viua mbegu za kiume (spermicides). Pia, kunywa dawa za kuua bakteria mwilini huweza kuua walinzi kwenye uke. Hii inaweza kuongeza hatari ya kupata maambukizi sugu ya njia ya mkojo.
    Kukoma hedhi: Kukoma hedhi husababisha mabadiliko ya homoni ambayo mwisho husababisha kubadilika kwa hali ya bakteria walinzi ndani ya uke hivyo kufanya wafe kwa wingi na uke kukosa ulinzi na kufanya iwe rahisi kupata maambukizi ya njia ya mkojo mara kwa mara.
    Aina za maambukizi ya UTI
    Maambukizi ya njia ya mkojo husababishwa na bakteria ambao mara nyingi huingia kwenye mfumo wa mkojo kupitia urethra na kisha kuzaliana na kuongezeka zaidi kwenye kibofu cha mkojo. Ili kuelewa zaidi maambukizi haya  namna yanavyotokea ni vizuri kugawanya maambukizi katika kibofu cha mkojo na maambukizi katika urethra.
    Maambukizi katika kibofu cha mkojo (Cystitis) mara nyingi husababishwa na bakteria waitwao Escherichia coli. E.coli ni bakteria wanaoishi kwenye utumbo wa watu na wanyama wenye afya nzuri. Bakteria hawa wakiwa mahala pao hawana madhara, isipokuwa wakipata upenyo wa kutoka huenda njia ya mkojo na kusababisha maambukizi.
    Mara nyingi hutokea pale mabaki ya kinyesi yasiyoonekana yanapoingia kwenye njia ya mkojo.
    Kushiriki ngono ya kinyume na maumbile kunaongeza hatari ya kupata maambukizi ya UTI.
    Maambukizi katika urethra (Urethritis) yanaweza kusababishwa na E.coli au magonjwa na maambikizi ya zinaa au yanayofahamika Sexually Transimitted Infections (STI) kama pangusa, kisonono au klamidia. Hata hivyo, magonjwa na maambukizi haya ya zinaa mara chache husababisha maambukizi ya njia ya mkojo.
    Dalili za Maambukizi sugu ya UTI
    Kwa mtu anayehisi maumivu chini ya kitovu au kwenye kibofu cha mkojo au mara kwa mara, kukojoa mkojo uliochanganyika na damu  ni dalili za wazi za maambukizi haya.
       Dalili zingine ni kutoa mkojo mzito, kuhisi kuchomwa au maumivu wakati wa haja ndogo na maumivu kwenye figo yaani chini ya mgongo au mbavu.
      Ikiwa maambukizi yatasambaa hadi kwenye figo, yanaweza kusababisha kichefuchefu, kutapika, baridi, homa kali (zaidi ya nyuzi joto 38.3), uchovu na kuchanganyikiwa.
          Mara nyingi, dalili hizi hutofautiana kati ya watoto na watu wazima. Umakini unahitajika kumbaini mtoto mwenye maambukizi haya.
    Wakati gani wa kumuona daktari?
    Mwanzoni, dalili za maambukizi ya njia ya mkojo zinaweza zisiwe zenye maumivu makali lakini baadaye yakawa makali kiasi cha kutovumilika na kuathiri shughuli za kila siku.
    Ikiwa dalili zitakuwapo kwa zaidi ya siku tano, inashauriwa ni vyema ukamuona daktari. Pia, muone daktari haraka ikiwa mwili utachemka sana, ikiwa una mimba au kisukari.
    Ikiwa una maambukizi sugu ya njia ya mkojo hii ina maana ulikuwa na maambukizi ambayo hayakutibiwa ipasavyo. Madaktari huwatuma wateja wao maabara kwa ajili ya vipimo zaidi kubaini ni maambukizi ya aina gani. Wataalamu wa maabara huangalia mkojo kupitia hadubini ili kuona bakteria wanaosababisha maambukizi.
    Kuotesha mkojo (urine culture test) ni kipimo kingine kinachoweza kufanywa na wataalamu wa maabara ili kubaini aina mahususi ya bakteria aliyemshambulia mgonjwa husika na mara nyingi  hurahisisha uchaguzi wa dawa kwa  daktari anayetoa tiba. Kipimo hiki huchukua siku moja mpaka tatu kabla majibu kutoka.
    Ikiwa daktari atahisi kuna uharibifu wa figo uliosababishwa na maambukizi hayo atapendekeza vipimo zaidi vya figo kama X-ray na Ultrasound. Kama una maambukizi yanayojirudia mara kwa mara daktari anaweza kufanya kipimo cha cystoscopy kinachohusisha mpira mrefu wenye lenzi mwishoni unaotumika kuangalia urethra na kibofu cha mkojo. Daktari anaweza kuangalia pia tofauti za kimaumbile alizonazo mwanamke zinazosababisha kujirudia kwa maambukizi.
    Madhara ya muda mrefu ya UTI                                
      Maambukizi sugu ya njia ya mkojo yanaweza kusababisha madhara  kwenye figo. Ugonjwa wa figo husababisha kuharibika kwa figo yenyewe na  kwa watoto wadogo, kusambaa kwa bakteria kwenye damu (septicaemia). Kwa wajawazito  huongeza hatari ya kuzaa watoto njiti endapo hautakabiliwa kwa wakati.
    Kujikinga na UTI  
    Kojoa mara nyingi uwezavyo muda wowote unapojihisi kufanya hivyo.
    Wakati wa kutawaza, safisha kwa kupeleka mkono nyuma. Kunywa maji mengi kusafisha bakteria kwenye njia ya mkojo kila mara unapokojoa bila kusahau kuvaa chupi iliyotengenezwa kwa pamba.
    Epuka kuvaa nguo za ndani zinazobana sana na kutumia diaphragm kama njia ya uzazi wa mpango.
    Tumia mafuta ya kulainisha wakati wa tendo la ndoa ikiwa inawezekana ili kuondoa michubuko isiyo ya lazima yenye kufanya upenyo wa bakteria.
    Kwa wanawake, epuka kuoga ndani ya mapovu mengi kwa kuwa kemikali zilizopo kwenye sabuni huingia kwenye uke na kuua bakteria walinzi hivyo kufanya iwe rahisi kupata maambukizi.
    Kwa wanaume, ikiwa haujatahiriwa osha vizuri uume wako mara kwa mara baada ya haja ndogo au tendo la ndoa.
    Scroll to Top