728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday 5 August 2016

    CHUNUSI| Fahamu sababu za chunusi na tiba yake kwa ufupi

    Chunusi ni nini?
    Chunusi ni sababu iliyozoeleka ya kutokea kwa mabaka kwa watu kuanzia umri wa miaka 12 na 25 na wakati mwingine kwa watu wenye umri zaidi ya hapo. Wavulana huathriwa zaidi kuliko wasichana na mara nying huathiri maeneo ya uso, mgongo, shingo na kifuani.
     Hali hii isipotibiwa inaweza kukaa kwa zaidi ya hata miaka 5 kabla ya kuondoka kabisa lakini pia kwa baadhi ya watu huweza kukaa zaidi.

    Nini Husabababisha Chunusi?

    Ijue Ngozi Kwanza kwa ufupi

    Kuielewa ngozi: Chini ya ngozi kuna tezi (Sebaceous gland) ambayo hufanya kazi ya kutengeneza mafuta mafuta ya ngozi (Sebum) . Pia kwenye ngozi kuna matundu madogo (pores) ambayo hurusu mafuta kutoka kwenye tezi kuja nje ya ngozi, pia kuna vinyweleo ambavyo vinaota kwenye matundu haya.
    Ukiwa kijana unatengeneza mafuta zaidi ya ngozi kuliko ukiwa mdogo na hii huchangiwa na ukuuaji na mabadiliko ya homoni mwilini au puberty ambayo huchochea kuzalishwa kwa mafuta
    Ni lazima kuwa kama mwili utatengeneza mafuta zaidi ngozi itakuwa ya mafuta zaidi yaani greasy na ndivyo hatari ya kupata chunusi inakuwepo. Baadhi ya watu hutengeneza mafuta haya mengi zaidi kuliko wengine.  
    Hatua za Chunusi: Baadhi ya vitundu huzibwa na mafuta yanapozidi mwilini na hii ni kwa sababu ngozi ya juu vitundu vinajaa mafuta na baadhi ya chembe hai za ngozi (skin dead cells) ambazo zinajazana kwenye vitundu kwa juu. Unaweza kuona sehemu ya uchafu (Pulgs) unaoziba vitundu kwa juu kama baka dogo lijulikanalo kama black heads na whiteheads (comedones)
    Angalizo: Baka au weusi unatokana na rangi ya ngozi au skin pigment na mara nyingi si chafu kama inavyofikiriwa. Mara nyingi chunusi haiwezi kukua zaidi ikishafikia hali hii ya comedones.
    Mara nyingine mafuta hujilundika chini ya vitundu vilivyozibwa, hali hii inapotokea huitwa pimples au papules na hii ni hatua isiyo hatari sana kwenye chunusi.
    Chunusi zilizokithiri: mafuta yanapozibwa husababisha baadhi ya bacteria kama Propioni bacterium acnes kukaa na kuzaliana kwenye vitundu vya ngozi na mara nyingi bacteria hawa huwepo kwenye ngozi bila madhara makubwa kwenye ngozi ila wakizidi huleta  Sasa wanapozidi hufanya mwili kupigana na hao bakeria na kusababisha uvimbe kwenye ngozi (Inflammation) na ngozi kuonekana nyekundu na vinundu kukua na kuwa na usaha (Pustules) na mara nyiningine hukua zaidi na kuonekana kama jipu (Nodules au cysts)
    Mara nyingi chunusi hizi hupona zenyewe na wakati mwingine huacha baka baada ya inflammation kuondoka nah ii huonekana zaidi kwa watu weusi Huacha vikovu vidogo huondoka taratibu na kuweza kuacha alama kwenye ngozi.

    BAADHI YA SABABU ZA CHUNUSI

    Maelezo ya juu ni namna chunusi inavyoweza kutokea, lakini pia baadhi ya magonjwa huweza kusababisha kutokea kwa chunusi kwa wanawake kwa mfano uvimbe kwenye yai au mirija ya uzazi pamoja na uzalishaji wa homoni za kiume kwenye yai la kike au tezi la adrenali.Hali hizi au magonjwa haya husababisha vinyweleo kusinyaa mbali na chunusi pia husababisha wingi wa vinyweleo (hairsutism). Vilevile kemikali pia husababisha kutokea kwa chunusi (Halogenated hydrocarbons)
    Kitu gani kinaongeza chunusi na kuleta madhara kwenye ngozi?
    ·         Vidonge vya majira.
    ·         Mabadiliko ya homoni kwa wanawake hasa wakati wa hedhi huleta vichunusi
    ·         Vipodozi na make ups huongeza chunusi lakini make up mara nyingi hazizidishi chunusi na inashauriwa kutumia vipodozi ambavyo havina mafutaau oil
    ·         Kutumbua chunusi kunaongeza uvimbe na madoa.
    ·         Kutoka jasho sana au hali ya hewa ya joto na unyevu, jasho jingi huziba vitundu vya hewa vya ngozi
    ·         Nguo kubana hasa vilemba na sidiria kutokana na jasho na msuguano
    ·         Utumiaji wa baadhi ya dawa kama phenytoin kwa ajili ya kifafa au cream na ointment za steroids.
    ·         Baadhi husema vyakula vyenye sukari na maziwa huongeza chunusi lakini hakuna uthibitisho wa kitaalamu kwenye hili.
    Some myths about acne-Ukweli dhidi ya uzushi kuhusu chunusi
    ·         Chunusi inasababishwa na kutooga,
    ·          Mawazo au stress yanaleta chunusi
    ·         Chunusi sio infection pekee bali ni mchanganyiko wa kubadilika kwa homoni za mwili, mafuta ya ngozi au sebum na bacteria wa ngozi kuwa wengi kuliko kawaida.. Chunusi haiambukizwi kwa kugusana
    ·         Huwezi kutibu chunusi kwa kunywa maji mengi.
    ·         Huwezi kutibu chunusi kwa kuota jua.
    ·         Wengine huamini kuwa chunusi haitibiwa na dawa, sio kweli kama ukitumia dawa vizuri unapona chunusi kabisa.
    Jinsi ya kutunza ngozi kwa mtu mwenye chunusi
    ·         Usioshe uso mara kwa mara, kwa kawaida mara mbili kwa siku inatosha sana. Tumia maji ya uvugu vugu kwani maji ya baridi au moto yatafanya hali ya chunusi kuwa mbaya zaidi. Usisugue uso sana na badala yake tumia kitambaa laini na
    ·         Kutumia sabuni zenye dawa (Antiseptic washes) husaidia.
    ·         Huwezi kuliondoa baka la chunusi kwa kusugua kwani ni sehemu ya ngozi yenye rangi  yaani skin pigment (melanin)
    ·         Baadhi ya cream husaidia hasa ambazo hazina manukato na zile zinazoleta unyevu kwenye ngozi (fragrance-free, water-based moisturising cream).  Usitumie cream zenye mafuta mengi kwani zinaziba vitundu vya hewa vya ngozi.

    Malengo ya kutibu chunusi: Malengo ni kuondoa mabaka na makovu kadri inavyowezekana. Tiba inaweza kuwa ya kupakaa au vidonge..
    Unaweza pia usitumie chochote kwa chunusi ambayo haijavimba na kuwa kubwa. Chunusi ndogo ndogo hazina madhara sana na hupata watu wengi bila kuwaharibu, ila chunusi zilizovimba na kweka kitu kama usaha sio nzuri na unaharibu uso na tiba ni muhimu kuzuia mabaka na makovu
    Dawa za kupakaa: baadhi ya gels, cream na lotion hutumika kutibu chunusi na hufanya kazi tofauti tofauti. Ni vyema kusoma kipeperushi cha dawa kabla hujaanza kuitumia na ni muhimu kuitumia eneo lililoathirika au kuzunguka eneo hilo pekee
    Benzoyl peroxide  inaweza kupakwa kwenye ngozi na inaua bacteria, kupunguza uvimbe wa chunusi na kupunguza kuziba kwa vitundu vya hewa vya  yaani to unplug blocked pores. Hupatikana kwa majina tofauti tofautiTherefore, it often works well to clear inflamed spots and it helps to clear bna nguvu kama: 2.5%, 4%, 5% na 10%
    Benzoyl peroxide:
    ·         Hubadili rangi ya nywele pamoja na baadhi ya vitambaa unavyotumia kupakaa.
    ·         Husababisha ngozi kuwasha na kama hali hiyo ikitokea unashauriwa kuacha kwa muda na kutumia yenye nguvu kidogo au punguza muda wa kutumia kwa siku badala ya mara mbili unaweza kupakaa mara moja kwa siku. Ili kupunguza kuwasha unatakiwa kufanya yafuatayo:
    ·         Wengi inawakubali yenye nguvu ya 5% kama ikileta madhara jaribu 2.5% na ukipenda yenye nguvu zaidi basi tumia kidogo kidogo.
    ·         Tumia iliyochanganywa na maji na sio  alcohol-based.
    ·         Pakaa kwa mara moja kila siku unapoanza kuitumia na baada ya masaa unaitoa na endelea kuongeza kidogo kidogo muda wa kuiacha kwenye ngozi.
    ·         Ikishakuzoea tumia mara mbili kwa siku.

    Retinoids ni nzuri kwenye kuondoa vitundu vilivyoziba. Ina majina mengi na inahusisha adapalene, tretinoin na isotretinoin ambazo huja kwa majina tofauti tofauti ya kibiashara. Husaidia pia kupunguza uvimbe wa chunusi. Unahitaji cheti kutumia dawa hizi. Unapotumia dawa hizi;
    ·         Unaweza kupata wekundu kwenye ngozi na wakati mwingine ngozi kubanduka lakini hali hurudi kawaida jinsi unavyoendelea kuitumia.
    ·         Mwanzoni inaweza kuzidisha chunusi lakini zitpungua unapoendelea
    ·         Unapozitumia hizi, usikae kwenye mwanga wa jua na vizuri ukazitumia usiku na kuosha
    ·         Madhara makubwa unapotumia hizi dawa au kemikali ni kuwashwa, kuungua au ngozi kuwa kavu. Hivyo unapoanza kutumia inakulazimu kutumia ambayo haina
    ·         Haitakiwi kuwa mjamzito unapozitumia kwani huweza kuathiri kiumbe cha tumboni.

    Antbiotics au Kemikali za kuua Bakteria: Zinapopakawa kwenye ngozi huua bacteria na kupunguza uvimbe wa chunusi. Lakini hazisaidii sana kwenye kuzibua matundu ya ngozi hivyo ni nzuri kwenye kutibu chunusi lakini hazisaidii kuondoa madoa doa. Hivyo hizi dawa hutolewa pamoja na cream au dawa zingine ili kutibu kabisa chunusi. Pia ni muhimu kuzitumia kwa tahadhari kwani bacteria zina tabia ya kuzoea hizi dawa na kwa baadae kushindwa kuziondoa (resistance)
    Azelaic acid huzibua vitundu vya hewa na haisababishi kuwashwa kwa ngozi kama retinoids na zinapunguza uvimbe pia lakini si kwa kiasi kikubwa kama.
    Mchanganyiko wa dawa husaidia sana kutibu kabisa chunusi na baadhi ya vipodozi unakuta zina benzoyl peroxide na antibiotic,au  retinoid na antibiotic. Mchanganyiko hufanya kazi zaidi kuliko dawa ikiwa pekee.
    Vidonge vya Antibiotics: Husaidia kuua bacteria, kupunguza uvimbe
    Hazisaidii sana kwenye kuzibua vitundu vya ngozi hivyo ni vyema kutumia na cream zenye benzoyl
    Tetracycline-based antibiotics ni nzuri kwa kutibu chunusi kuliko zingine na hizi ni kama vile; oxytetracycline, tetracycline, doxycycline na lymecycline.
    ·         Watoto chini ya miaka 12 hawtakiwi kutumia hizi antibiotics za tetracycline.
    ·         Kwa wajawazito, wanaonyonyesha au unategemea ujauzito hushauriwi
    ·         Chakula na maziwa zinazuia kufanya kazi kwa oxytetracycline au tetracycline. Hivyo ni vyema kuzinywa kabla ya kula na tumia maji badala ya maziwa. Doxycycline na lymecycline hizi unaweza kuzinywa hata ukiwa umekula teyari.
    Antibiotics Zingine ni erythromycin na trimethoprim.
     Tiba kwa njia ya homoni
    Vidonge vya majira (The combined contraceptive pill) zinaweza kusaidia iwapo chunusi zako zimetokana na mabadiliko ya homoni kwa mfano chunusi zinazojitokeza ukubwani au wakati wa hedhi.
    Ni homoni ya oestrogen ambayo ipo kwenye kidonge cha majira ndio inayosaidia.  Kidonge chenye co-cyprindiol, husaidia pale inapobainika  homoni ya androgen imesababisha chunusi.Kwa mfano kukua kwa nywele usoni pamoja na chunusi co –cyprindol inafaa kwani ina mchanganyiko wa oestrogen na cyproterone (ant androgen)
    Isotretinoin hupunguza kuzalishwa kwa mafuta ya ngozi (sebum) ambayo inatengenezwa na sebaceous glands. Hufanya kazi vizuri kwa kuondoa mabaka hata yale sugu. Hata hivyo hutumiwa baada ya ushauri wa mtaalamu.
    Ni muda gani unahitaji kutibu chunusi ?
    Ili uanze kuona maendeleo mazuri kwa tiba yoyote utalazimika kutumia kwa mwezi mzima na maendeleo mazuri huonekana baada ya wiki ya sita au zaidi. Chunusi nyingi haziishi kwa sababu watu wengi hufikiria chunusi hutibiwa kwa siku kadhaa hivyo huacha tiba
    Hivyo ni vyema kutumia dawa au kipodozi kwa wiki sita kabla ya kumua kuacha au kusema hakija kusaidia. Ni vyema kubadili dawa kama hakuna matokeo mazuri au kuongeza dawa au kipodozi kwenye kile ulichoanza na usiache kabisa.

    Je, Chunusi inaweza kurudi baada ya Tiba?

    Ukiacha tiba chunusi hurudi ni vyema kuendelea na tiba mpaka ziishe kabisa. Kwa watu wengine hutumia mpaka miaka 5 kuweza kupona kabisa au kufikia umri mkubwa wa kuacha kuzalisha sebum. Tumia  benzoyl peroxide au topical retinoid kama muendelezo wa tiba ya chunusi.
    Antibiotics hutumiwa mara moja na baada ya hapo endeleza kupakaaa kwenye ngozi dawa zilizotajwa hapo juu

    Je unahitaji kwenda hospitali kwa ajili ya chunusi?


    Chunusi isipopona unashauriwa kwenda hospital na kumuona daktari, pia baadhi ya makovu huweza kuondolewa na dakatri mtaalamu na ngozi yako kuonekana vizuri.
    Nashukuru kwa kupitia makala hii naumefaidika na kitu..Siku njema!
    Prepared by: Buswelu pharmacy +255767650213
    Ilemela, Mwanza
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: CHUNUSI| Fahamu sababu za chunusi na tiba yake kwa ufupi Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top